Zimebaki dakika 4 kumaliza sura

Yaliyomo

Nguzo Iliyosahaulika

Sura 24 · 4 dakika za kusoma

Mustakabali wa Kanuni za Msingi

Tayari tumesoma nukuu ifuatayo kutoka kwa sura “Msingi wa Imani yetu”. Ni moja ya maono ya mbeleni ya Dada White ya matengenezo makubwa ambayo yangetokea miongoni mwa Waadventista Wasabato; mageuzi haya yangejumuisha kuacha Kanuni ya Msingi. Hivi ndivyo shirika jipya litakavyoanzishwa.

Ellen G. White:

Adui ya roho ametaka kuleta dhana kwamba matengenezo makubwa yangetukia kati ya Waadventista Wasabato, na kwamba matengenezo haya yangefanyika yangejumuisha kuacha mafundisho ambayo yanasimama kama nguzo za imani yetu na kuhusika katika mchakato wa kujipanga upya. Je, matengenezo haya yangefanyika, matokeo yangekuwa nini? Kanuni za ukweli ambazo Mungu katika hekima yake ametoa kwa kanisa la masalio zingetupwa. Dini yetu ingebadilishwa. Kanuni za msingi ambazo zimeendeleza kazi kwa miaka hamsini iliyopita ingehesabiwa kama makosa. Shirika mpya lingeanzishwa. Vitabu vya namna mpya vingeandikwa. Mfumo wa falsafa ya kiakili ingeanzishwa. Waanzilishi wa mfumo huu wangeenda katika miji na kufanya kazi ya ajabu. Sabato, bila shaka, ingechukuliwa kuwa nyepesi, kama vile Mungu aliyeiumba. Hakuna kitu kingeruhusiwa kusimama katika njia ya harakati mpya. Viongozi wange-fundisha kwamba wema ni bora kuliko uovu; lakini Mungu akiondolewa, wangeweka utegemezi wao kwa nguvu za kibinadamu, ambazo, bila Mungu, hazina thamani. Msingi wao ungejengwa juu ya mchanga, na dhoruba na tufani zingefagilia mbali muundo.

Lt242-1903.13; 1903
Ellen G. White:

Nani mwenye mamlaka ya kuanzisha harakati hizo? Tuna Biblia zetu. Tuna uzoefu wetu, unaothibitishwa na utendaji wa kimiujiza wa Roho Mtakatifu. Tuna ukweli ambao haukubali kufifiwa au kubati-lishwa. Je, hatutakataa kila kitu ambacho hakipatani na ukweli huu?

Lt242-1903.14; 1903

Ellen White saw the effort of the enemy to remove these Fundamental Principles. They have sustained the work from the beginning. They were truths attested by the miraculous working of the Holy Spirit, and they admit no compromise. Shall we not repudiate everything that is not in harmony with this truth?

Ellen White aliona juhudi za adui kuondoa Kanuni za Msingi ambazo zimedumisha kazi tangu mwanzoni. Zilikuwa kweli zilizothibitishwa na kazi ya kimiujiza ya Roho Mtakatifu, na hazikubali maafikiano. Je, hatutakataa kila kitu kilichopo ambacho haipatani na ukweli huu?

Ellen G. White, 1913
Ellen G. White, 1913

Dada White alitutabiria wakati ujao. Tunatazama utimilifu wake leo. Kulinganisha Kanuni za Msingi na Imani za Msingi za leo, tunaona kwamba dini yetu imebadilika. Imani yetu kuhusu Umbile la Mungu imebadilika. Vitabu vya agizo jipya vimeandikwa, ambvayo havina msingi wa Neno thabiti la Mungu. Mfumo wa falsafa ya kiakili imeanzishwa.

Matengenezo haya yalifanyika katika wakati wake. Hivi ndivyo alivyoeleza siku za Kanisa la Waadventista Wasabato katika wakati wake na katika siku zijazo:

Ellen G. White:

Wakati huu ni wakati mzito na wa kutisha kwa kanisa. Malaika tayari wamejifunga mshipi, wakingoja agizo la Mungu la kumimina mabakuli yao ya ghadhabu ulimwenguni. Malaika wa kuangamiza wanachukua kazi ya kisasi, kwa maana Roho wa Mungu anajiondoa polepole kutoka kwa ulimwengu. Shetani pia anakusanya majeshi yake ya uovu, akiwaendea ‘wafalme wa dunia na wa ulimwengu mzima,’ kuwakusanya chini ya bendera yake, ili kuzoezwa kwa ajili ya ‘vita vya siku ile kuu ya Mungu Mweza Yote.’ Shetani anapaswa kufanya jitihada zenye nguvu zaidi kwa ajili ya ustadi katika mzozo kuu wa mwisho. Kanuni za msingi zitatolewa, na maamuzi yatafanywa kuhusiana nazo. Mashaka yanatawala kila mahali. Kutomcha Mungu kunazidi. Imani ya washiriki binafsi wa kanisa itajaribiwa kana kwamba hakuna mtu mwingine duniani...

Ms1a-1890.8; 1890

Juhudi zenye nguvu zaidi za Shetani ni kuondoa Kanuni za Msingi kwa kuzifunika mashaka ndani. Kwa kuzingatia mtazamo wa leo tunashuhudia ukweli wa unabii wa Ellen White .

Ellen G. White:

Nawaambia sasa, ya kwamba nitakapolazwa, mabadiliko makubwa yatatokea.

Ms1-1915.2; 1915

Swali la kweli tunalo sisi wenyewe ni, wakati Kanuni za Msingi zinapokuwa zikitolewa, nitafanya uamuzi gani juu yao? Je, hatutakataa kila kitu ambacho hakipatani na kanuni hizi? Utafanya uamuzi gani?

The early voice of prophecy
Foretold of dangers that might be.
"The devil plots," it was declared,
"To steal the truths that we once shared."

The Principles, so strong and sure,
Our God designed them to endure
But now the sands shifts ‘neath our creed,
Because God’s voice we did not heed.

Ideas new are masked as light,
Removing pillars, which were right.
Rewritten books, with theories new
As skeptics veil that which was true.

Shall Sabbath lose its sacred glow?
Shall we forget the God we owe?
"Foundations crumble," so it seems,
As truth is lost to prideful dreams.

Look back to days, our early start,
Where truths divine were etched in heart.
But now the devil’s strategy
Erodes the truth which used to be.

Dear brethren, to the past return,
For early faith, our hearts must yearn.
For warnings plain, and visions sent,
Designed from error to prevent.

Stand firm in storm as tempests roar,
Reclaim the truths worth fighting for.
The voice of Ellen, stark and clear:
"Reject the false, the truth hold dear.

Now chose, as battle lines are drawn
Make sure God’s side you’re standing on.
Stay on the paths cast up of old,
God’s fundamentals, firmly hold.