Zimebaki dakika 5 kumaliza sura

Yaliyomo

Nguzo Iliyosahaulika

Sura 20 · 5 dakika za kusoma

Dr. Kellogg na maandiko ya Ellen White

Dk. Kellogg alidai kwamba katika The Living Temple aliwakilisha hisia sawa zilizo-tetewa na Dada White. Vivyo hivyo, leo wengi wanadai kwamba Dada White alikuwa mfuata utatu na anawajibika kwa kukubali kwa kanisa fundisho la Utatu1. Dada White mwenyewe, alitangaza madai hayo kuwa ya uongo.

Ellen G. White:

Adui anatafuta kuingiza miongoni mwa watu wa Mungu nadharia za kimizimu, ambazo zikikubaliwa, zingedhoofisha msingi wa imani ambayo imetufanya kuwa tulivyo. Anawaongoza watu kuwasilisha hadithi zillizovikwa na Maandiko. Wapo wanaodai kwamba maandishi ya Dada White yanapatana na mafundisho haya. Natangaza kuwa hii ni uongo. Watu wanaweza kutumia Maandiko vibaya; wanatafsiri vibaya maneno yangu; lakini Mungu anaelewa mipango yao. Ninashukuru jinsi gani kwa hili! Adui anapoingia kama mafuriko, Roho wa Bwana atatuinulia kiwango juu yake.

Ms137-1903.21; 1903

Dk. Kellogg alitetea nadharia ambazo zingekubaliwa zingedhoofisha msingi wa imani yetu. Ni muhimu kuelewa kwa usahihi kile kinachofanya msingi wa imani yetu, ambayo Dada White alirejelea. Tumeona kwamba inarejelea Kanuni za Msingi. Kuangalia katika maandishi yake, na maandishi ya waanzilishi wetu, tunaona kwamba fundisho la Utatu linapingana na Umbile la Mungu na ukweli kuhusu uwepo wa Mungu. Leo, na fundisho la Utatu kama sehemu ya imani yetu, tunatambua kwamba tumetoka kwenye Kanuni za Msingi na kuunda msingi mwingine. Dada White hakuhusika na mabadiliko haya. Ni tafsiri isiyo sahihi ya kazi zake. Maandishi yake hayavunji msingi wa imani ambayo imetufanya tulivyo. Kazi yake ya baadaye inapatana kabisa na ukweli uliotolewa hapo mwanzo.

Ellen G. White:

Miaka hamsini iliyopita haijafifisha yodi moja au kanuni ya imani yetu kama tulivyopokea ushahidi mkubwa na wa ajabu ambao ulifanywa kuwa uhakika kwetu mnamo 1844, baada ya kupita kwa wakati. ... Hakuna neno limebadilishwa au kukataliwa. Ambacho Roho Mtakatifu alishuhudia kama ukweli baada ya kupita kwa wakati, katika kukatishwa tamaa kwetu kuu, ni msingi imara wa ukweli. Nguzo za ukweli zilifunuliwa, nasi tukakubali kanuni za msingi ambazo zimetufanya tulivyo—Waadventista Wasabato, wazishikao amri za Mungu na kuwa na imani ya Yesu.

Lt326-1905.3; 1905

Upotoshaji wa msimamo wa kanisa

Kwa kupotosha maandishi ya Dada White, Dk. Kellogg hakupotosha kazi yake tu, lakini msimamo rasmi wa kanisa unaoonyeshwa katika Kanuni za Msingi. Ellen White alimkemea Kellogg kwa kupotosha msimamo wa kanisa. Tunaposoma karipio hili, tukumbuk msimamo wa sasa wa kanisa juu ya Umbile la Mungu kama inavyolinganishwa na hatua ya kwanza ya Kanuni za Msingi.

Ellen G. White:

Wewe si timamu katika ukweli. Kauli zako zilizopewa kwa waumini na makafiri imetuwasilisha vibaya sisi kama watu ambao hawakuibadili kweli kwa upotofu. Kauli hizo hufifisha ushawishi ambao Mungu angetutaka tuwe nao mbele ya ulimwengu katika kufunua kwa wazi, kwa lugha isiyo na shaka kwamba sisi ni wa kusimama kidete kwa kanuni za imani yetu na kwamba sisi tunashikilia mwanzo wa imani yetu imara hadi mwisho. Sisi ni shirika madhubuti! Tunaamini mnamo 1903 kweli zile zile tulizoamini tulipoanzisha Sanitarium na Chuo pale Battle Creek, na tunajua kwamba hatukuwa na ‘makama’ au ‘mana’ kuhusu hili jambo.

Lt300-1903.4; 1903
Ellen G. White:

Wakati umewaambia mambo uliyo nayo na kutoa kauli ulizo nazo hapo awali kwa wasioamini, moyo wangu umekuwa na huzuni kweli. Umethibitisha kuwa umeondoka kutoka kwa imani. Maneno yale yale uliyoyasema mbele ya watu wenye ushawishi wa kidunia, kama karatasi zimeripoti maneno yako, zimewasilishwa kwangu wazi kutoka kwa midomo yako kama wewe wamezungumza nao. Hatuwezi kufanya kazi kukupa ushawishi kama mtu ambaye tunaweza kukwamini kazi takatifu inayohusiana na taasisi zetu, kwani unahitaji kwanza kuokoka na kuongozwa.

Lt300-1903.5; 1903
Ellen G. White:

Wewe si timamu kiimani. Nimeeleza haya katika shajara yangu miezi kadhaa iliyopita. Kwa hakika umeweka watu wa Mungu, ambao Bwana amewaongoza hatua kwa hatua katika njia za ukweli na kuwekwa juu ya msingi imara, kwa upotovu mbele ya makafiri. Baadhi wameiacha imani na wataendelea kupotosha kazi ambayo Mungu alinipa.

Lt300-1903.6; 1903
Ellen G. White:

Swali la patakatifu ni fundisho lililo wazi na dhahiri kama tulivyolishikilia kama watu. Kwa hakika hauko wazi juu ya ubinafsi wa Mungu, ambao ni kila kitu kwetu kama watu. Hakika umemwangamiza Bwana Mungu Mwenyewe.

Lt300-1903.7; 1903
Ellen G. White:

Kwa nini uchukue uhuru wa kutoa kauli ulizotoa, kana kwamba ulikuwa na mamlaka ya kusema hivyo, ikiwa ni uwongo? Umesababisha ukweli wa imani yetu kukosa maana mbele ya makafiri, na ukweli ambao unapaswa kudumishwa kwa umaarufu na kuinuliwa na watu hawa, umekaana na kupuuza katika kauli zako nyingi. Ulithubutu vipi kufanya hivi? Inatulazimu sasa kuwasilisha msimamo wetu wa kweli ambao unatufanya sisi kuwa Waadventista Wasabato. Ushawishi wowote ambao Mungu alikupea hapo awali imekuwa katika rehema kwako, kwa kukuangazia nuru.

Lt300-1903.8; 1903
Ellen G. White:

Hatuwezi kwa wakati wowote ule kuwa na upotoshaji wowote juu ya haya maneno mazito na masomo muhimu ya ukweli ambayo yamekuwa imani ya watu wetu tangu 1844. Hii ina maana kubwa kwetu. Bwana angetaka nikuambie kwamba adui, kupitia kwa madanganyo ya ajabu, ameweka kutokuamini akilini mwako, na umedhihirisha hiyo waziwazi. Wote wanaopokea mawasilisho yako wataingia kwenye njia za ajabu ikiwa wataunganishwa nawe. Unaleta ndani moto wa ajabu, wa kawaida, lakini si moto wa kuwasha wa Mungu mwenyewe; na sasa lazima nizungumze kwa uwazi kwa watu wetu kwamba Bwana ametuongoza hatua kwa hatua na alituonyesha mwanga wa wazi juu ya patakatifu pa mbinguni katika patakatifu pa patakatifu sana ambapo Mungu alijidhihirisha yeye kwa wateule wake.

Lt300-1903.9; 1903

Dk. Kellogg alipotosha ukweli uliokuwa msingi wa imani yetu; haswa kwa wingi, aliwakilisha vibaya ukweli juu ya Umbile la Mungu, ambao ulikuwa kila kitu kwetu sisi kama watu. Ikiwa mnamo 1903, ililazimu kuwasilisha msimamo wetu wa kweli ambao unatufanya sisi kuwa Waadventista Wasabato, je, ni muhimu zaidi kwetu leo? Dada White alifanya sehemu yake katika kushikilia msingi wa imani yetu hapo mwanzo, lakini inaonekana ni kama tumeshasahau.

In faith’s foundation, once so clear,
Dear Ellen’s words, we should revere.
J.H. agreed, yet in deceit,
And twisted truth, in his conceit.

The enemy—dear Ellen warned—
Will twist beliefs, till they are scorned.
These dangerous theories, wrongly dressed,
In Scripture’s garb, the false impressed.

"False!" she declared, against the tide,
His crafty statements were denied.
Defense was strong, her vision, broad
The Fundamental were from God.

No word was changed, not peg nor pin,
From when the pillars did begin.
Now who would dare to move a board—
This platform built up by the Lord.

For Kellogg’s stance did not agree,
Foundation was not trinity.
God’s personality is true;
Confusion came through Kellogg’s view.

Yet, Ellen stood, unyielding, firm,
The early truth she did confirm.
Against the tide of Trinity
She held the truth of deity.

Today, as then, let’s hold the line,
The early pioneer faith, divine.
Truth’s legacy, let’s rightly claim,
Unchanging, solid, still the same.

The way God led, let’s not forget,
These principles are firmly set.
Against the changing winds of doubt,
Her writings guide, within, without.

Tanbihi

  1. 1
    William Johnsson, Adventist Review, January 6th, 1994, ‘Present Truth –Walking in God's Light